Friday 26 April 2013

UFASIHI UNAOJITKEZA KATIKA JUMBE FUPI ZA SIMU ZA MKONONI



 FASIHI YA AFRIKA

DONDOO
1.     UTANGULIZI
-         Fasili ya dhana za msingi
-         Mjadala kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa Thieta ya jadi ya Kiswahili
2.     MADA
-         Thieta ya jadi ya Kiswahili ni nini/ipi
-         Sifa za Thieta ya jadi ya Kiswahili/Kiafrika
3.     HITIMISHO



Makala hii inakusudia  kubainisha sifa za thieta ya jadi ya Kiswahili /Kiafrika,lakini kabla ya kujikita katika mada yenyewe, dhana za msingi zitafafanuliwa kwanza ili kumwezesha msomaji kuelewa akutanapo na dhana hizo katika makala hii. Dhana hizo ni pamoja na miviga, drama/tamthiliya na sanaa za maonesho/thieta.
Kerr(1995:1) anasema; Drama refers to displays of actions to an audience, in which there is an imitation of events in the real or supernatural world and there is an element of story or suspence.
Kwamba, Drama ni kuonesha matendo kwa hadhira,ambapo kuna kuiga matukio halisi au matukio ya kimiujiza na kuna elementi ya hadithi au taharuki. (Tafsiri yetu)
Ni matendo yanayoletwa mbele ya hadhira na ndani mwake kuna kuiga matukio katika hali halisi au ya kidhahania.
Kerr(1995:1) akifasili miviga anasema; Ritual  refers to an action which is undertaken to give homage to,obtain assistance from,or in some way intercede with supernatural forces. This may or may not involve dramatic representation.
Kuwa, ni kitendo kinachofanyika kwa lengo la kutoa heshima, kupata msaada,au kwa namna fulani kuomba nguvu za kimiungu. Hii inaweza kuhusisha au isihusishe uigizaji (Tafsiri yetu)
Naye Wamitila (2003:128) katika Kamusi ya Fasihi,Istilahi na Nadharia anasema Miviga ni dhana inayotumika kuelezea sherehe ambazo aghalabu hufanywa katika kipindi maalumu katika jamii fulani. Aghalabu sherehe hizi hufanywa kwa sababu mbalimbali,kwa mfano, huweza kufanywa ili kumtoa mtu kutoka kundi moja la kijamii hadi jingine.
Sanaa za maonyesho zinajumuisha zile sanaa ambazo huwasilisha ,ana kwa ana, wazo kwa hadhira kwa kutumia usanii wa kiutendaji. Mlama (1983:186) 
Pia anasema ni kitendo chochote chenye sifa za mchezo,mchezaji, uwanja wa kuchezea na watazamaji.

Kerr (1995:1)   anasema; Theatre cover drama, many forms  of ritual, dance,and other perfoming arts such as acrobatics,mime and semi dramatized narratives.
Thieta hujumuisha drama,miviga,dansi,na sanaa nyinginezo za vitendo kama vile sarakasi,uigizaji bubu na simulizi za kidrama( Tafsiri yetu)
Mabweazara (uk 11) naye anasema, Theatre can be defined as an activity in which an actor takes a role other than himself and through mime, speech, song and dance movements conveys or communicates a message to an audience, this is an aspect that has always been deeply ingrained in African life styles.(kutoka tovuti)
Thieta inaweza kufasiliwa kama kazi ambapo mwigizaji anachukua uhusika zaidi ya yeye mwenyewe kupitia uigizaji bubu, maneno, nyimbo na miondoko ya kimuziki kuwasilisha ujumbe kwa hadhira. Kipengele hiki kinafungamana na mtindo wa maisha ya Mwafrika.(Tafsiri yetu) 
Pamoja na kwamba wataalamu mbalimbali hutumia dhana ya drama na tamthiliya kumaanisha kitu kilekile,tunaweza kusema kuwa kuna utofauti kwa kiasi fulani  ambapo usanii wa kiutendaji katika drama hutegemea zaidi vitendo na uongeaji tofauti na ilivyo katika tamthiliya ambayo inakuwa imeandikwa kwa lengo la kuoneshwa kwa hadhira.
MJADALA KUHUSU KUWEPO AU KUTOKUWEPO KWA THIETA YA JADI YA KISWAHILI/KIAFRIKA
Kuna mitazamo miwili kuhusu uwepo wa thieta ya jadi ya Kiswahili/Kiafrika
          I.  Mtazamo wa Kimagharibi (Eurocentric view)
          Ii. Mtazamo wa Kiafrika (Afrocentric view)
I.                   Mtazamo wa Kimagharibi
Mtazamo huu unawahusu wanazuoni mbalimbali, baadhi yao ni Ruth Finegan, Adande, Dadi na Burton. Wao wanasema Afrika haikuwa na kitu kinachoitwa sanaa za maonesho kama Ulaya, kwani sanaa hizo zilihusisha sehemu maalumu ya kuoneshea(ukumbi), ulipaji wa kiingilio kwa hadhira, fanani kulipwa, mazoezi kwa ajili ya maonesho na matangazo mbalimbali katika vyombo vya habari kama redio, runinga, na magazeti/majarida.

Hata hivyo wanasema kama ilikuwepo basi ni kidogo sana, au la iilikuwa katika hatua changa sana (tete). Finegan(1970:500) anasema; It would perhaps be true to say that in Africa,in contrast to Western Europe and Asia, drama is not typically a wide-spread or a developed form.
Katika mjadala wa Lo Lyong mwaka 1975 kuhusu sanaa za maonyesho za jadi anasema hakuna kitu kigeni kiutamaduni  Afrika kama wazo la sanaa za maonesho. Anaendelea kusema kuwa Uli Beier, ambaye anajua zaidi kuhusu utamaduni wa Wayoruba kuliko Myoruba yeyote anasema wazi kuwa hakuna sanaa za maonesho zilizojisimika katika mila na desturi za Wayoruba.
Wanazuoni hao na wengine wenye mawazo hayo ni wale wanaochambua utamaduni wa Mwafrika bila ya kuhusisha na utaratibu mzima wa kuzalisha mahitaji muhimu ya maisha. Ikiwa Mwafrika siku zote amekuwa akijishughulisha katika harakati hizi, vipi tuseme hakuwa na sanaa zake? (Bakari 1995: 3)
II.                 Mtazamo wa Kiafrika
Unahusisha wanazuoni mbalimbali, baadhi yao ni Penina Mlama, Leshoai, Kerr, Lihamba,Mukotani Rugyendo na Ebrahim Hussein. Wao wanathibitisha uwepo wa sanaa za maonesho kwa kutumia ushahidi wa majigambo unaopatikana katika ukanda wa ziwa mfano Bahima na Bahaya, miviga, ngoma na utambaji hadithi nk.
Mlama (1991:56) anatoa mfano wa majigambo toka Bahaya kama ifuatavyo;
                                   I am a tough character
                                   My soul is likened to a tobacco leaf

                                   My heart to a wooden spoon

                                  Which of the two is better
                                  It is you my lord the king who worries my mind
                                  I am totaly commited to defending the kingdom
Kwa ujumla wataalamu hawa wenye mtazamo wa Kiafrika wanasema sanaa za maonesho ni dhana inayojitegemea bila ya kulinganishwa na kitu chochote kutoka nje, Hivyo ni zao la jamii husika.
CHANZO CHA MJADALA HUO
Chanzo cha  mjadala huo kilitokana na nadharia ya ulinganishi (comparative approach) iliyolinganisha vitu kwa kuzingatia chimbuko, athari na raghba(interest) na pia tatizo hili limetokana na kutumika kwa lugha ya Kiingereza katika kufafanua dhana za thieta ya jadi. Ili kuweza kutatua mgogoro huu sharti kwanza wanazuoni wa Kiafrika wajadiliane na wafanye utafiti juu ya istilahi muafaka zitakazotumika kufafanua sanaa za maonyesho za Afrika.
 Ricard(2000:14) anasema; A debate on the existence of theatre in Africa was raging in the West. Kwamba mjadala kuhusu uwepo wa thieta Afrika ulianzia kwenye nchi za kimagharibi( tafsiri yetu)
Hivyo basi,kwa hoja hizo, sisi kama wanakikundi tunaungana na mtazamo wa Kiafrika kwamba thieta ya jadi ya Kiswahili ilikuwepo. Katika kufanya hivyo,tutabainisha sifa za thieta ya jadi ya Kiswahili, jambo ambalo makala hii inakusudia kushughulikia.  
Ikumbukwe kwamba Sanaa za maonesho katika Tanzania ya leo ziko za aina mbili, yaani sanaa za maonesho ya jadi na sanaa za maonesho mamboleo. Sanaa za maonesho ya jadi ya Kiswahili ni zile ambazo zina chanzo na msingi katika jamii ya Tanzania. Sanaa hizi ni pamoja na ngoma, majigambo, sherehe za jando na unyago,matambiko na ngomezi. Katika shughuli hizi watu hufanya vitendo vya kisanaa kama vile uchezaji ngoma, uimbaji,upigaji muziki, utongoaji mashairi,vikiambatana na matendo ya mwili na matumizi ya lugha.
Vitendo hivi vya kisanaa ni njia mojawapo bora ya kuwasiliana kati ya watu na watu wengine au miungu na mizimu katika jitihada za kuyakabili mazingira na kuendeleza jamii. Kwa kucheza ngoma watoto hufunzwa tabia inayotegemewa katika utu uzima, kwa kuimba miungu huelezwa matatizo ya ukame,magonjwa nk, kwa kusimulia hadithi watu hufunzwa historia ya jamii ,tabia nzuri,jinsi ya kuishi na watu wengine, kwa kuimba na kufanya vitendo vya kuigiza wenye tabia mbaya hukosolewa na kurekebishwa .
Hatar A.(2001:4) akimnukuu Mlama(1983)  anasema ; We are using theatre not in the Western Classical tradition of stage, perfomers and an audience, but in the more general form of “symbolic perfomance, with symbolic images representing life through action”. Such symbolic perfomance could include dance,storytelling,poetic recitations, some rituals, dramatizations and so on.
Hatutumii thieta kwa misingi ya Kimagharibi ya kuwepo kwa jukwaa,watendaji na hadhira bali kwa namna ya kijumla zaidi ya kutumia watendaji kiishara kwa picha za kiishara kuwakilisha hali halisi ya maisha kivitendo. Utendaji huo unaweza kujumuisha dansi,utambaji hadithi,miviga,drama nakadhalika.( tafsiri yetu)   
Semzaba(1973:5)  anasema;  sanaa za maonesho za jadi ni zile sanaa ambazo hazijaathiriwa wala kuingiliwa kwa mtindo wowote na namna yoyote. (Tafsiri yetu)
Kwa upande mwingine, sanaa za maonesho mamboleo ni zile zinazotokana na athari za ustaarabu wa kigeni  hususan tamthiliya ambayo ililetwa kwetu na Waingereza wakati wa ukoloni, awali kwa lengo la kujifurahisha na kujikumbusha maisha ya kwao. Mlama (1976:38) Si lengo la makala hii kujadili aina hii ya sanaa za maonyesho. Lengo hapa ni kujadili sifa za thieta  ya kijadi ya Kiswahili/Kiafrika.
Sanaa za maonesho za jadi zilifungamana na kazi za kila siku za jamii husika. Mabweazara(uk 11) anasema; indigenous African theatre was deeply rooted in day-to-day activities. It was part and parcel of the whole conception of existence,and it was also a communal activity. It existed within its functional context, and it sought to perpetuate the virtues of society and purge all evil. 
Naye Semzaba (1973:5) anasema; Thieta ya jadi ya Kiswahili ilifungamana na  mifumo iliyoimarika vya kutosha au uumbaji wa sanaa ulio imara katika jamii, na uwepo wa utamaduni au tamaduni kwa maendeleo ya mifumo hii katika makundi hayo ya kijamii.(Tafsiri yetu)
Sanaa za maonyesho za jadi zilikuwa na sifa ya kuonekana kimatendo. Mlama (1976: 188) anasema kwa bahati mbaya sanaa za maonyesho za jadi zilipigwa vita zaidi ya vipengele vingine vya utamaduni wa wenyeji hasa kwa sababu sanaa hizi zilionekana kimatendo.
Pia  sanaa za maonesho za jadi zilijisimika katika utamaduni, mila na desturi za jamii husika. Mlama(1976:190). Kama tulivyoona kuwa thieta ya jadi ya Kiswahili inafungamana na kazi za kila siku na maisha kwa ujumla, ni wazi kabisa kwamba ni vigumu mila,desturi na utamaduni wa jamii husika kuepukika katika thieta ya jamii hiyo.
Pre-colonial Tanzania’s theatres therefore were part and parcel of the people’s way of life, and the perfomances were in direct responce to the people’s interpretation of meaningful phenomena.
Kwa hiyo sanaa za maonesho za anzania kabla ya ukoloni zilikuwa ni sehemu ya maisha ya watu, na matendo yalikuwa ni matokeo ya moja kwa moja ya tafsiri ya watu juu ya matukio ya kweli katika maisha(Tafsiri yetu)
Vilevile Mlama 1983:4 anasema Pre-colonial African theatre was essentially utilitarian and sought to raise,discuss and impart societal norms, as well as be able to them on to successors generations. This was not art for arts sake, but art for specific,or as we would now say, specific purposes.
Kimsingi sanaa za maonesho za jadi zilikuwa na lengo maalumu lililokusudiwa kuibua, kujadili na kuathiri mila za kijamii na kuweza kuzirithisha kwenye vizazi vinavyofuata. Hii haikuwa sanaa kama sanaa tu, bali sanaa kwa kusudi maalumu.(Tafsiri yetu)
Pia anasema kuwa utendaji katika sanaa hizo ulikuwa shirikishi,and often the audience merged with the performers, and anyone with a spark of inspiraion cold pick up the song wherever.
Naye Kerr (1995:2)  anasema kuwa:  the notion of a communal,sharing,pre-colonial society has found a theatrical equivalent in an aesthetics emphasis on African theatre’s anonymous,participatory qualities in contrast with divisive individualism of colonial Western theatre. Mbweazara (uk 12) anasema unlike in the Western forms of theatre, the audience in the Chiware ceremony is part of the entire activity-it does not watch from without but participates actively in the entire ceremony.
Vilevile thieta ya jadi ya Kiswahili ilikuwa mali ya jamii nzima. Hii ni kutokana na kwamba ilichukuliwa kama sehemu ya kazi za kila siku.
 Kerr (1995:5) anawasisitiza  wanathieta wa kiafrika kugeuka na kutumia mbinu ya thieta ya jadi ya collectivity’socialism’. Anasema;
                  There are clear homologies here with political theories urging a return to pre-colonial communocratic values.
Pia tamthiliya za jadi za Kiswahili ziliendana na ngoma na miviga. Ngoma ni pamoja na sherehe, utawala na taratibu nzima. Ngoma inahusishwa na nguvu fulani ambapo nguvu hiyo ina imani fulani.
Thieta za jadi ya Kiswahili  ilifungamana na dini za kijadi, mizimu na miungu. Matambiko mbalimbali yalifanyika kwa lengo la kuiomba miungu mambo mbalimbali kama vile mvua na kujiepusha na balaa na magonjwa mbalimbali. Hii inafungamana moja kwa moja na ontolojia ya Kiafrika.
Vilevile thieta ya jadi ya Kiswahili ilifungamana na muktadha kutegemea na na shughuli nzima ya wakati huo,hakukuwa na ukumbi maalum wa kwa ajili ya sanaa za maonesho . kwa mfano, ngoma ilichezwa kulingana na kusudi la wakati huo na mahali ambapo ngoma hiyo inakusudiwa ktoa funzo fulani wakati huo kwa hadhira fulani.
 Mulokozi (1996:190) anasema hapa Afrika, kumbukumbu  za kwanza za maigizo ya kitamthiliya tunazipata Misri,ambako michezo ya miviga iliyohusu kufa na kufufuka kwa Mungu wa Wamisri aliyeitwa Osiris ilikuwa ikiigizwa kila mwaka. Anaendelea kusema kuwa mbali na drama za kimisri ambazo huenda ziliandikwa,maigizo yasiyoandikwa hapa Afrika yalikuwa ni sehemu ya matendo mengi ya kijamii, hasa katika miviga na ngoma. Halikadhalika ,tamthiliya bubu(mime), maigizo ya watoto na maigizo ya watani yalikuwepo tangu zamani. Mulokozi anasema kuwa hata hivyo drama hizi zilifungamana na fasihi simulizi, hazikuwa za kibiashara, hazikurasmishwa na hazikuandikwa. Tamthiliya zilizoandikwa ili ziigizwe rasmi jukwaani ni matokeo ya athari ya tamthiliya za Ulaya.
Katika kipengele cha kurasimishwa, tunaona kwamba kuna utata kwa sababu kila jamii ilikuwa na fani maalumu zilizotumika katika jamii hiyo kwa lengo maalumu. Kwa mfano jamii ya Wahaya ilikuwa na majigambo ya ushujaa.
Mulokozi (1996:211) akijadili suala la thieta ya umma, anasema kuwa mbinu za sanaa za maonesho za jadi zilitumika, na baadhi ya mbinu hizo ni; Nyimbo na ngoma, Lugha sadifu kulingana na mazingira, Maudhui yanayoakisi maisha na matatizo ya watu wenyewe na    yanayoendeleza maslahi yao, Ushirikishwaji wa mtu yeyote badala ya wataalamu tu katika sanaa na Matumizi ya ishara, maigizo-bubu, na mbinu nyingine za kijadi.
Kwa ujumla sanaa za maonesho za Kiafrika ni dhana inayotendeka, na ili dhana hiyo itendeke inahitaji mambo yafuatayo; Dhana inayotendeka mfano ngoma, tambiko, miviga na nyimbo, Mtendaji –hapa itategemea kinachotendeka mf manju,kungwi na ngariba, Uwanja wa kutendea hapa inategemea na dhana inayotendeka, kwa kawaida jukwaa hubadilika badilika , Watazamaji ambapo watazamaji wanaweza kuwa na nafasi mbili ya utazamaji na yautendaji. Mfano mtazamaji anaweza kushiriki kuimba wimbo,kucheza na kupiga vigelegele ili kuonesha kilele chake cha furaha.
Vipengele hivi ni kwa mujibu wa Mlama(1981:153). Mulokozi anakubaliana na vipengele hivyo  na kuongeza kipengele cha ubunifu na kusudio la sanaa hiyo.
Semzaba (1973:5) anasema; Thieta ya jadi ya Kiswahili ilifungamana na  mifumo iliyoimarika vya kutosha au uumbaji wa sanaa ulio imara katika jamii, na uwepo wa utamaduni au tamaduni kwa maendeleo ya mifumo hii katika makundi hayo ya kijamii.(Tafsiri yetu)
Hivyo basi, tunaweza kuhitimisha mjadala wetu kwa hoja kwamba, thieta ya jadi ya Kiswahili ilikuwepo na ilifungamana na kazi za kila siku. Suala la kutokuwepo kwa sanaa za maonesho Afrika kwa mtazamo wa kimagharibi halina mashiko kutokana na nadharia ya ulinganishi na dhana walizotumia. Jamii huwa zinatofautina katika nyanja mbalimbali za maisha, hakuna jamii zinazofanana. Hivyo tunapendekeza zitumike dhana ambazo zinawakilisha thieta ya Kiswahili/ Kiafrika badala ya kutumia dhana za Kimagharibi, pamoja na kujikita katika misingi ya thieta ya jadi ya kiswahili ili kuondoa utata uliopo.




MAREJEO
Bakari J. A na Materego G.R (1995),  Sanaa kwa maendeleo: Stadi, Mbinu na
                                             Mazoezi, Amana Publishers, Dar es salam.
Etherton M. (1982),  The Development of African Drama; Africana Publishing
                                   Company, New York.
Finnegan  R (1970),  Oral literature in Africa; Oxford University Press, Nairobi.
Hatar A (2001),  ‘The state of Theatre Education in Tanzania’, prepared for
                              UNESCO, University of Dar es salaam.
Kerr D (1997) ,  African  Popula Theatre by David Phillip Publishers(pty) ltd,
                            Claremont 7735 Cape Town.
Mlama P (1981) ,  ‘Sanaa za maonesho katika jamii ya asili’  katika Omari C.K
Na M.Mvungi; Urithi wa utamaduni wetu, Tanzania Publishing House,
                           Dar es  salaam
Mlama P. (1991),  Culture and Development; The Popular Theatre Approach,
                                 Uppsala, Nordiska Afrikainstitutet.
Muhando P. na Balisidya N.(1976) , Fasihi na Sanaa za Maonesho, Tanzania  
                                                              Publishing House, Dar es Salaam.
Ricard A. (2000),  Ebrahim Hussein : Swahili Theatre and Individualism na Nyota
                               Publication, Dar es Salaam
Semzaba, E. (1973),  Trends in Modern African Theatre movement, M.A Thesis,
                                University of Dar es Salaam


No comments:

Post a Comment

soma na uelewe